Watu 30 walazwa hospitalini Mombasa kutokana na ugonjwa wa chikungunya
Watu 30 wamelazwa kwenye hospitali
mbali mbali za kaunti ya Mombasa pwani mwa Kenya baada ya kuugua ugonjwa
wa Chikungunya, kwa mujibu wa shirika la habari la serikali KBC.
Gavana
wa Mombasa Hassan Joho, amezindua magari matano yenye mashine na dawa
kunyunyisiwa katika kaunti hiyo wakati ugonjwa unazidi kuwatishia watu
zaidi.Chini ya miezi mitatu iliyopita kaunti ya Mombasa ilikuwa ikikabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo watu kadha walilazwa hospitalini na maeneo kadhaa ya mankuli kufungwa katika kaunti hiyo.
Joho alithibitisha kuwa kumekuwa na visa 120 vya wagonjwa na imethibitwa kuwa visa 32 kati ya hivyo ni vya ugonjwa wa chikungunya.
Kufuatia ugonjwa huo kusambazwa na mbu Gavana Joho amewashauri wenjeji wa mombasa kushirikiana kwa karibu na serikali ya kaunti kuondoa mazingira salama kwa mbu.

No comments